Na Leonard Magomba

Jumla ya Wafanyakazi 265 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wamenufaika na mafunzo maalumu ya maandalizi ya kustaafu.

Mafunzo hayo yanayotolewa na TPA kwa kushirikiana na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yamelenga kuwandaa watumishi hao na maisha ya baadae baada ya kustaafu, amesema Bi. Concepter Kadula, wakati anafungua rasmi mafunzo hayo.

“Menejimenti imeandaa mafunzo ya maandalizi ya kustaafu kwa watumishi wetu wapatao 265 ambao wametimiza umri wa kustaafu kuanzia miaka 55 na kuendelea,” amesema Bi. Concepter Kadula.

Bi. Kadula ambaye alifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa TPA alisema kwamba lengo la mafunzo haya ni kuwawezesha wastaafu watarajiwa waweze kujiandaa kwa kuweka mipango wezeshi ili kuyamudu maisha ya baadae baada ya kustaafu.

Aidha, alisema kwamba menejimenti ilifanya hivi baada ya kubaini kuwa watumishi wengi huingiwa na hofu pindi muda wa kumaliza utumishi wao unapokaribia.

“Hii hofu inatokana na kutojiandaa vema kimaisha kwa kuwekeza katika miradi midogo midogo ambayo itasaidia katika kuingiza kipato na kuweza kumudu maisha ya kila siku baada ya kustaafu.

Menejimenti imeona ni vema kupata mafunzo haya ili yawaweke sawa kisaikolojia kwa kuwa na mtazamo chanya juu ya kuyaendea maisha mapya baada ya kustaafu utumishi wa umma.

Kwa mujibu wa mratibu wa mafunzo hayo kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma, Bw. Felicianus Richard amesema katika mafunzo hayo watatoa elimu kuhusu mipango na mikakati ya kustaafu, elimu ya Afya na utunzaji wa fedha, mtindo bora wa maisha na ujasiriamali.

Elimu nyingine iliyotolewa katika mafunzo hayo yaliyofanyika Bagamoyo ni pamoja na jinsi ya kuanzisha miradi inafaa na kutembelea miradi mbalimbali na kuona namna ya uanzishwaji na uendeshwaji wake ili tuweze kujifunza.

Mwisho

Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Bw. Plasduce Mbossa akijibu hoja mbalimbali toka Kamati ya Bunge ya Miundombinu mjini Dodoma

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Juma Kijavara akifafanua jambo wakati akijibu hoja mbalimbali toka Kamati ya Bunge ya Miundombinu mjini Dodoma

The renovation and upgrading of the Tanga Port have started yielding positive results as the facility is next month poised to host the largest ship ever docked at the port. According to Tanga Port authorities, the development follows completion of the first phase of the major improvements project by 100 per cent and the second phase, which has reached 93 per cent. Tanga Port Manager Masoud Mrisha told the ‘Daily News’ that as the work nears completion, the port is expected to handle the largest ever ship on March 15th this year -MV Metsovo from US, which will dock at the port with 50,066.147 metric tonnes of petroleum bulk petcock. According to the port manager, the cargo will go to Sayona Chemicals and Neelkanth Chemicals Limited. “Before the upgrading and renovation of the port, these kinds of ships were handled through stream operations but now the vessels will dock at the berth and serve quickly and efficiently,” Mr Mrisha said. He further detailed that, the port is also expected to host another ship in early March this year with 5,000 tonnes of fertiliser (Ammonia Nitrate), the cargo which had never been handled at the port. The Port Manager added that the port is also set to handle 2,481 tonnes of copper, which will pass through the facility to DR Congo. “This is a good indication that our port is going to handle goods which have never passed through it,” he said. The port manager said the first phase of the project which was implemented at a cost of 172.3bn/- involved expansion of the entrance channel, increase of the draft at the turning basin and procurement of modern equipment. On the other hand, Mr Mrisha said the implementation of the second phase of the project involved the construction of new 450-metre-long berths at a cost of 256.8bn/-. Mr Mrisha further noted that the port has also surpassed its cargo volume target for January this year which was 67,000 tonnes to 77,000 tonnes, noting that they are confident to attain 3 million target of cargo volume per year upon completion of the project. He added that for the 2021/2022 financial year the port had a target of handling 714,800 tonnes of cargo but it surpassed its target by serving 986,000 tonnes. According to Mr Mrisha, currently the port has the capacity of handling 750,000 tonnes of cargo but upon completion of the project the volume is expected to increase to 3 million tonnes per year. He said increased efficiency will be another benefit of the project because numbers of days for cargo handling are going to be reduced from five to three depending on the size of the cargo. “The port is currently having modern equipment for cargo handling and also the ships will now be docking at the port so they will be handled quickly and efficiently,” Mr Mrisha said. “The safety of the goods will also be enhanced because there will be no more stream operations and the goods which had never been handled at the port will now be passing through the facility such as vehicles,” he said. The port boss expressed gratitude to President Samia Suluhu Hassan for dishing out the funds for execution of the crucial project which will not only stimulate economic growth of Tanga Region but also open up social economic opportunities in other northern regions including Kilimanjaro, Arusha and Manyara Source DailyNews online
The Tanzania Port Authority (TPA) has contributed to the construction of a girls' dormitory at Kilindoni Secondary School located in Mafia District, Pwani Region. Mafia’s District Commissioner, Mr. Martine Stephen Mtemo has received the help presented by the Small Port Manager, Mr. Erasto J. Lugenge on behalf of the Director General of TPA Mr. Plasduce Mbossa and thanked TPA for contributing significantly to the development of Mafia District. The Head of the District has said that the economy of his District depends on the Port Industry and asked the Authority to continue helping the Mafia to solve the challenges of its citizens. Along with the support, TPA also built Mafia jetty in 2007 and donated Aluminum windows in 2019 for the construction of Kirongwe Health Center in Mafia district

Mkurugenzi Mpya wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Mrisho S. Mrisho

Na Levina Msia

Mkurugenzi Mpya wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Mrisho S. Mrisho amefungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Bandari ya Dar ea Salaam na kubainisha vipaumbele vyake ili kuongeza ufanisi.

Katika kikao hicho ambacho ni cha kwanza tangu ateuliwe kushika nafasi ya Ukurugenzi wa Bandari hiyo, Mkurugenzi huyo alibainisha vipaumbele vyake vinavyolenga kuongeza ufanisi katika utendaji bandarini hapo.

Miongoni mwa vipaumbele alivyoainisha kuvisimamia kwa haraka ni pamoja na kuongeza kasi ya upatikanaji wa vitendea kazi, uboreshaji wa maeneo ya utendaji kazi, kuhakikisha upatikanaji wa vifaa vya ofisi na maeneo mbalimbali ya shughuli za utekelezaji.

vingine ni pamoja na kuisafisha Bandari kwa kupanga vyema yadi za kuhifadhia shehena,  kuvuka malengo ya kiutendaji, kutoa motisha kwa wafanyakazi wanaofanya vizuri, kuimarisha kitengo cha ‘welfare’ ili kukabiliana na matatizo ya ndani ya wafanyakazi, kusimamia kwa karibu michakato ya manunuzi kwa lengo la kufanikisha upatikanaji wa mahitaji muhimu kama vile vipuri na uboreshaji wa Viwanja vya Michezo.

Wajumbe wa Baraza wameahidi kumpatia ushirikiano Mkurugenzi wa Bandari na kumhakikishia kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo ya Taasisi na Serikali kwa ujumla.

Mwisho

Tanzania Ports Authority (TPA) has taken over the cargo handling services done by the Tanzania International Container Services (TICTS) Limited effectively as from 01 January, 2023. Thus, all related TICTS documents will be available at the Info Center menu above.

Na Leonard Magomba

Wafanyabiashara toka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), wamefanya ziara ya kutembelea Bandari ya Dar es Salaam ili kujionea miundombinu ya Bandari hiyo pamoja na kukagua maboresho mbalimbali yaliyokwishafanyika na yanayoendelea kufanyika.

DRC ambalo ndilo soko kuu kwa Bandari ya Dar es Salaam hutumia Bandari hiyo kupitisha bidhaa mbalimbali haswa za madini ya aina mbalimbali yanayopatikana nchini humo, sambamba na mazao ya misitu.

Kwa upande wa bidhaa zinazoingia kutoka katika soko la kimataifa, DRC inapitisha bidhaa za nafaka, magari, mitambo, mavazi, vinywaji, mafuta na bidhaa za chuma.  

Kabla ya ziara ya kutembelea miundombinu ya Bandari, wafanyabiashara hao walifanya mazungumzo katika ukumbi wa mikutano uliopo jingo la TPA Tower na menejimenti ya TPA chini ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Dkt. Lufunyo Hussein.

Katika mazungumzo hayo, Dkt. Lufunyo aliwakaribisha na kuwashukuru kwa kuendelea kuiamini na kutumia Bandari za TPA hususani Dar es Salaam, Tanga na Kigoma kupitisha shehena mbalimbali zinazoingia na kutoka nchini DRC.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi Mkuu alitumia fursa hiyo, kuwahakikishia usalama wa mizigo yao na utayari wa TPA kuendelea kutoa huduma bora na zenye ufanisi zaidi kwa wafanyabiashara hao kwa maslahi mapana ya nchi zote mbili.

Akifafanua kuhusu Ulinzi na Usalama, Dkt. Lufunyo aliwaeleza wafanyabiashara hao jinsi mifumo ya kisasa ya Ulinzi na Usalama inavyofanyakazi ambapo alisema TPA imefunga takribani Kamera 400 za CCTV kuzunguka eneo la Bandari nzima ambazo zinafanyakazi saa 24.

Akizungumza kwa niaba ya ujumbe wa wafanyabiashara hao kutoka nchini DRC katika miji ya Kalemie, Uvira, Bukavu na Goma, Mwenyekiti wa Umoja huo aliishukuru TPA kwa huduma bora zinazotolewa katika Bandari hiyo.

Mwenyekiti huyo alisema kwamba, kwasasa mizigo yao inahudumiwa kwa ufanisi na kuwafikia kwa wakati.

Pia alipongeza kuwa siku 30 huru zinazotolewa na TPA kwa wafanyabiashara wa DRC pasipo kutozwa tozo ya kuhifadhia mizigo (storage charges) imesaidia wafanyabiashara hao wa DRC wanaotumia Bandari hizo kupunguza gharama za kupitisha Shehena kwenda katika miji hiyo.

Mwenyekiti huyo, aliwahakikishia TPA kuwa wafanyabishara hao toka nchini DRC wapo tayari kuendelea kufanyabishara na Bandari za TPA kwani zimekuwa na unafuu mkubwa wa gharama na wenye faida mtambuka kwa pande zote ukilinganisha na Bandari shindani.

mwisho

Subcategories