BANDARI YA DAR ES SALAAM IMEPOKEA MELI YENYE WATALII 516 ‘THE CRYSTAL SYMPHONY’
Bandari ya Dar es Salaam, terehe 2 Januari 2026 imepokea meli ya kitalii inayoitwa The Crystal Symphony ikiwa na watalii 516 ambao wametembelea vivutio mbalimbali hapa nchini.
Wakala wa Meli hiyo Bw. Gilbert Nikata, amesema meli hiyo ya kifahari inaurefu wa mita 238 kina cha mita 8 imefika Bandari ya Dar es Salaam ikitokea Msumbiji, itakaa kwa siku moja na kuelekea Zanzibar.
Pamoja na mambo mengine ameipongeza Serikali kupitia TPA kwa maboresho makubwa yaliyofanyika katika Bandari hiyo pamoja na huduma bora bandarini hapo na kuahidi ujio wa meli nyingine zaidi za kitalii.
EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"