BARAZA DOGO LA BANDARI ZA ZIWA VICTORIA LAFANYA KIKAO CHA 61
Bandari za Ziwa Victoria zimefanya kikao cha 61 cha Baraza Dogo la Majadiliano, kilichoongozwa na Mwenyekiti, Bw. Gerald A. Kifaro ambaye ni Kaimu Meneja wa Bandari hizo.
Katika kikao hicho, wajumbe walijadili kwa kina masuala mbalimbali, yakiwemo maendeleo na mafanikio ya Bandari za Ziwa Victoria pamoja na maslahi ya wafanyakazi, kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi na ustawi wa Mamlaka.
Aidha, Baraza lilifanya uchaguzi wa Katibu na Naibu Katibu, ambapo wajumbe walipata fursa ya kuchagua viongozi watakaoendesha shughuli za Baraza hilo kwa ufanisi zaidi.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mwenyekiti Bw. Gerald A. Kifaro aliwasisitiza viongozi waliochaguliwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu, na kuzingatia kanuni pamoja na taratibu za uendeshaji wa mabaraza.
Kwa ujumla, Bandari za Ziwa Victoria zinaendelea kujikita katika kuimarisha ushirikiano wa ndani, uwajibikaji na maendeleo endelevu kwa manufaa ya Mamlaka na wadau wake.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"