Sélectionnez votre langue

Wafanyakazi Bandari ya Dar es Salaam wamepongezwa kwa kuhudumia shehena tani Mil. 13.99 kwa kipindi cha miezi mitano, kuanzia Julai mpaka Novemba 2025 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Pongezi hizo zimetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed G. Abed wakati akifungua Kikao cha 75 cha Kamati ya Utendaji Bandari ya Dar es Salaam, kinachofanyika mjini Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Amesema kuwa kipindi kama hiki cha miezi mitano 2024/2025, Bandari ya Dar es Salaam ilihudumia shehena tani mil. 10.48 ikiwa ni tofauti ya tani 3.51 sawa na 33.5%.

Ameongeza kwa kusema kuwa, kwa mwenendo huo inatarajiwa mpaka kufika mwisho wa mwaka 2025/2026 Bandari ya Dar es Salaam itahudumia tani mil.32.

Aidha Bw. Galus amesema kuwa mafanikio hayo yametokana na juhudi kati ya Menejimenti ya Bandari ya Dar es Salaam na Wafanyakazi kwa kushirikiana na Wadau na wawekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam yanayopelekea kufikia malengo ambayo Bandari ya Dar es Salaam imewekewa na Serikali.

Kikao cha Kamati ya Utendaji kitakaa kwa siku mbili, kikifuatiwa na Kikao cha 75 cha Baraza la Wafanyakazi kituo cha Bandari ya Dar es Salaam kitakachofanyika tarehe 16 Januari 2026.