Sélectionnez votre langue

Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed Gallus Abed amekutana na Wadau na watumiaji mbalimbali wa Bandari hiyo katika kikao kilicholenga kusikiliza na kutatua changamoto zinazohusiana na shughuli za kibandari.

Kikao hicho cha siku moja kimefanyika Februari 14,2025 katika Ukumbi wa mikutano wa Bandari ya Dar es Salaam, kimehitimishwa kwa Bw.Gallus kuwataka wadau kushirikiana katika kutatua changamoto mbalimbali zinazoathiri ufanisi wa Bandari pamoja na kuhakikisha maazimio ya kikao hicho yanatekelezwa.