TIMU YA MPIRA WA WAVU YA TPA YANYAKUWA NAFASI YA PILI

Timu ya Mpira wa Wavu ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Bandari Wanawake, imenyakuwa nafasi ya pili katika michuano ya ligi ya Mpira wa Wavu Taifa iliyochezwa katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.
Bandari Wanawake katika mchezo wake wa fainali imecheza dhidi ya Prisons na kupoteza kwa seti 0-2, matokeo yaliyowaweka TPA kutika nafasi ya pili katika michuano hiyo.
Kwa upande wa Bandari Wanaume, bahati haikuwa upande wao ambapo waliishia katika hatua ya robo fainali katika mchezo uliochezwa Septemba 25, 2025, dhidi ya timu ya Jeshi Stars.
Kwa upande wa Tuzo, Mchezaji Gaudencia Paulo wa Bandari Wanawake ametunikiwa tuzo ya Mzuiaji bora wa mipira ( Best liberal )