Sélectionnez votre langue

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inashiriki Kongamano la Kitaifa la Wadau wa Uchumi wa Buluu 2025, linaloenda sambamba na maonesho ya shughuli zinazofanywa na Taasisi shiriki, na linafanyika kwa siku mbili Jijini Dar es Salaam.

Kongamano hilo linaloenda na kauli mbiu ya “Bahari Yetu,Fursa Yetu, Wajibu Wetu: Kuanzia 2021 hadi 2025”, limefunguliwa Septemba 10, 2025 na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Abdallah Mhawi.

Kwa upande wa Maonesho, Banda la TPA limekuwa kivutio kwa Wadau mbalimbali wa Uchumi wa Buluu kutembelea kwa ajili ya kupata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka na shughuli mbalimbali za utekelezaji Bandarini.

Uchaguzi 2025 Logo