VINGOZI WA MENEJIMENTI YA TPA WATEMBELEA BANDA KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Viongozi wa Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa nyakati tofauti wametembelea Banda la TPA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ( Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Viongozi hao ni Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano Dkt. George Fasha na Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed Gallus Abed, wameeleza kuridhishwa kwao na elimu ya kuhusu shughuli za kibandari inayotolewa bandani hapo na kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi.
Banda la TPA katika maonesho ya Sabasaba lipo Katika Kitalu namba 42 Mtaa wa Mataifa ambao pia wapo Waendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, Kampuni za DP World na TEAGTL.