Sélectionnez votre langue

Maafisa wanafunzi 28 kutoka chuo cha Kijeshi cha Zambia Defence Service Command and Staff College (CSC) wakiongozwa na Kanali Sylvester Kakoma, tarehe 01 Oktoba,2025 wametembelea Makao Makuu ya Mamlaka ya Usimamzi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa ziara ya kujifunza.

Maafisa hao wakisindikizwa na Kanali Robert Mbuba pamoja na Maafisa wengine wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wameishukuru Menejimenti ya TPA kwa mapokezi mazuri na elimu waliyoipata kuhusu shughuli mbalimbali za kibandari, na mchango wake katika biashara na usafirishaji wa kimataifa.

Katika ziara yao hiyo, wamepokelewa na Menejimeni ya TPA ikiongozwa na Mkurugenzi wa Mipango, Ubora na Vihatarishi Dkt. Boniphace Nobeji na Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano Dkt. George S. Fasha, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu Bw. Plasduce Mkeli Mbossa.

Uchaguzi 2025 Logo