JUMA LA HUDUMA KWA MTEJA NCHINI RWANDA

Katika kuadhimisha Juma la Huduma kwa Mteja 2024, Ofisi ya Mamlaka ya Usimamizi ya Bandari Tanzania (TPA) Nchini Rwanda imewatembelea Wateja wake katika Jiji la Kigali na kuwapa zawadi mbalimbali kama ishara ya kushukuru kwa uhusiano mwema uliopo katika shughuli za kibandari kati ya Tanzania na Rwanda.
Afisa mwakilishi wa TPA Nchini Rwanda Bw. Adam Shindo ameongoza ziara za kutembelea Wateja hao na kuahidi kuimarisha zaidi Viwango vya Huduma kwa Mteja ili kuvutia Wateja zaidi kulingana na kauli mbiu ya “Above and Beyobd” na kuongeza mchango wa Ofisi hiyo katika Mafanikio ya TPA.