Select your language

Bandari ya Mtwara imeendelea kupongezwa kwa ufanisi mkubwa wa kuhudumia shehena mbalimbali ikiwemo shehena zenye kemikali.

Pongezi hizo zimetolewa tarehe 25 Machi, 2025 na Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Tanzania Profesa Said Vuai, kufuatia Bodi hiyo kufanya ziara katika Bandari ya Mtwara ambapo imeshuhudia shughuli mbalimbali za utekelezaji zikiendelea.

Kaimu Meneja wa Bandari ya Mtwara Bw. Mtunze Mwarabu Sudi amesema Bandari hiyo imeendelea kushirikiana vema na Ofisi ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika kutekeleza shughuli mbalimbali za kuhudumia shehena.