Select your language

Wadau wa Bandari ya Tanga wameipongeza Menejimenti ya Bandari hiyo, kwa juhudi kubwa walizofanya kuhakikisha kunakuwa na meli za moja kwa moja za shehena ya Makasha.

Wadau hao wametoa pongezi hizo wakati wa Kikao cha Kamati ya Maboresho ya Bandari ya Tanga (Port Improvement Committee - PIC) kilichojumuisha wadau mbalimbali kutoka Sekta binafsi na Taasisi za Serikali.

Wadau hao wamesema uwepo wa meli ya Makasha ya moja kwa moja kutoka nchini Irani mpaka katika Bandari ya Tanga itaondoa changamoto ya muda mrefu ya Bandari ya Tanga kupokea meli ndogo ndogo ‘Feeder ‘kutoka Bandari za nchi jirani ambazo zimekuwa zikisababisha Shehena nyingine kukosa nafasi katika meli hizo.

Kwa upande wake, Meneja wa Bandari ya Tanga, Bw. Salehe Mbega amewataka wadau hao kuwasilisha changamoto zao kwa wakati pindi zinapojitokeza ili kuhakikisha wateja wanapata huduma bora wakati wote.