BARAZA KUU LA WAFANYAKAZI TPA KATIKA KIKAO MJINI BAGAMOYO

Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) leo tarehe 19 Machi 2025, limefanya kikao chake cha Thelathini na Saba (37) mjini Bagamoyo Mkoa wa Pwani, kinacholenga kujadili na kuthibitisha Mapendekezo ya mpango wa Bajeti ya Mamlaka kwa mwaka wa Fedha 2025/ 2026 pamoja na Kupitia na kuthibitisha Kumbukumbu za Kikao cha Thelathini na Sita (36) kilichofanyika tarehe 2 - 3 Oktoba,2024.
Baraza hilo limeongozwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dkt. Baraka R. Mdima ambapo awali Baraza hilo lilitanguliwa na Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Baraza kuu la Wanyakazi kilichoongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu na Utawala Bw. Mbarikiwa Masinga kwa niaba ya Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dtk. Baraka R. Mdima.