Select your language

Baraza la Majadiliano (JIC) la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Kituo cha Bandari ya Dar es Salaam limefanya kikao cha kawaida cha pili (2) kinachofanyika mjini Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Kikao hiko cha siku (3) kimeanza tarehe 27 Februari 2025 ambapo kimelenga Kupitia na kuthibitisha kumbukumbu za kikao Na.1/2024/2025 cha Baraza la majadiliano ‘JIC’ kilichofanyika tarehe 16 mpaka 17/10/2024.

Kikao hiko kimeongozwa na Meneja Zimamoto na Usalama Bandari ya Dar es Salaam Bw. Mussa Biboze kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed Gallus.