MABORESHO YA MFUMO WA UENDESHAJI BANDARI

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inapenda kuujulisha Umma, Wateja na Wadau wa Huduma za Kibandari wa ndani na nje ya Tanzania kuwa, kutakuwa na maboresho ya mfumo wake wa Uendeshaji Bandari (TOS) siku ya tarehe 11 April 2025 saa 4 usiku hadi saa 7 usiku. Maboresho haya yataathiri huduma katika bandari ya Dar es Salaam kwa huduma za meli, vilevile bandari ya Tanga na Mtwara kwa huduma za meli na mzigo.