Select your language

Chama cha Wafanyakazi wa Shughuli za Meli na Bandari (DOWUTA) tawi la Makao Makuu, kimekamilisha mchakato wa Uchaguzi wa nafasi mbalimbali za chama hicho Januari 30,2024.

Katika uchaguzi huo uliokuwa na hamasa kubwa tofauti na miaka iliyopita,ambapo mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti ni Bw.Felician Hasunga na Bw. Isaac Mtamba akiibuka mshindi katika nafasi ya Katibu Mkuu.

Nafasi zingine zilizokuwa zinagombaniwa ni nafasi ya Uwakilishi wa Vijana wanaume ambapo Bw. Shamte Luwali na Bw. Omary Khalid walifungana kwa kulingana idadi ya kura na hivyo uchaguzi wa nafasi hiyo itarudiwa, huku kwa upande wa Vijana wanawake mshindi ni Bi. Hilda Shundi.

Nafasi tano Wajumbe wanawake washindi ni Bi. Irene Mmari, Bi. Mary Mahinya, Bi. Queen Chiwanga, Bi. Caroline Urio na Bi. Mariam Namota.

Washindi wa nafasi za uwakilishi wa idara ni Bw. Zubeir Sungura, Bw. Aloyce Kakusa, Bi. Esther Mchomvu, Bw. Calist Nyaki, Bw. Atufigwegwe Mwanjala, Bw. Mutasa na nafasi ya mweka hazina wa chama imechukuliwa na Bw. Adili Mindolo.