Select your language

Serikali ya Jamhuri ya Ireland imeeleza dhamira yake ya kuendeleza ushirikiano wa kibiashara na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Bandari za Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa Machi 14 2025 na Waziri wa Nchi, Mashauri ya Kigeni na Biashara wa nchi hiyo Mhe. Naele Richmond alipokutana na Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es Salaam.

Katika salamu zake za ukaribisho Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dkt. Baraka Mdima amesema, maboresho makubwa yaliyofanyika katika Bandari zote nchini yamechangia kuongeza ufanisi katika uhudumiaji wa shehena.