SALAMU ZA POLE

Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti na Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), tunaungana na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuomboleza vifo vya Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), pamoja na dereva wake, Muhajir Mohammed Haule. Tunatoa pole kwa familia, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko, watumishi wa TANESCO, ndugu, jamaa na marafiki.
Mwenyezi Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi.