TPA YAKABIDHIWA CHETI CHA PONGEZI KWA UWASILISHAJI BORA PSSF
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (Mb), ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa uwasilishaji bora wa michango na utoaji wa huduma kwa wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).
Mhe. Sangu ametoa pongezi hizo Februari 09, 2026, wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC), jijini Arusha, ambapo alikabidhi cheti cha pongezi kwa TPA. Cheti hicho kilipokelewa na Afisa Rasilimali Watu Mkuu wa TPA, Bi. Edna Kitila.
EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"