Serikali ya Jamhuri ya Msumbiji imeeleza nia yake ya kuendeleza na kukuza ushirikiano uliopo baina yake na Tanzania haswa katika sekta ya Uchukuzi kupitia Ushoroba wa Kusini.
Hayo yamejiri katika Mkutano baina ya Waziri wa Uchumi na Uchukuzi wa Msumbiji Mhe. Basilio Muhate na Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) uliofanyika Mei 06,2025 Makao Makuu ya TPA jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika Mkutano huo Mhe.Muhate amesema ushirikiano katika sekta ya Uchukuzi baina ya nchi hizi utaunganisha Bandari za Mtwara na Nacala hali itakayosaidia ukuaji wa Uchumi wa nchi zote mbili.
Waziri huyo amesema nchi yake ina miundombinu ya kutosha inayoweza kutumika ipasavyo katika shughuli za Uchukuzi wa shehena kupitia Ushoroba wa Kusini.
Awali wakati akitoa salamu za ukaribisho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Naibu Mkurugenzi Mkuu Dkt.Baraka Mdima, amesema shehena katika Bandari za Tanzania zinasafirishwa kwa njia ya Barabara na reli za TAZARA na Shirika la Reli la Tanzania (TRC) na mchakato wa ujenzi wa gati la kuhudumia meli za kitalii katika Bandari ya Dar es Salaam, upo katika hatua za mwisho.

TPA inawatakia Wanafunzi wote wa Kidato cha Sita kote Nchini, kila la kheri katika Mitihani ya kuhitimu Elimu ya Sekondari.
Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe Hemed Suleiman Abdulla kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 30 Aprili 2025, amefungua rasmi Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Mawakala wa Forodha Afrika Mashariki na Kati unaofanyika Kisiwani Unguja, Zanzibar na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa katika sekta ya forodha ili kuchochea maendeleo ya biashara na uchumi wa dunia.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliohudhuriwa na mamia ya wadau kutoka mataifa mbalimbali, Mhe Abdulla amesema Serikali ya Tanzania Bara na Visiwani zimejipanga kuboresha zaidi mazingira ya biashara kwa kuimarisha mifumo ya forodha, Miundombinu ya Uchukuzi katika nyanja zote ,kupunguza vikwazo vya kikodi na visivyo vya kikodi sambamba na matumizi ya teknolojia ya kisasa ili kuhakikisha huduma bora na za haraka kwa mustabali mpana wa Uchumi wa Tanzania na nchi jirani zinazotumia bandari za Tanzania.

Katika kusisitiza dhamira njema ya Serikali, amesema, Tanzania Bara na Zanzibar, zimewekeza katika miundombinu ya kisasa kama vile bandari, reli na barabara ili kuhakikisha ufanisi wa huduma za forodha na usafirishaji wa shehena.
Kwa upande wake Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa, amesema Tanzania inaendelea kuimarisha miundombinu ya uchukuzi ili kuifanya nchi kuwa kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Naye Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt Khalid Salum Mohammed, amebainisha kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatekeleza mikakati ya kuimarisha bandari na mifumo ya forodha visiwani humo kwa lengo la kuifanya Zanzibar kuwa lango muhimu la biashara za kimataifa.
Awali Rais wa Shirikisho la Kimataifa la Mawakala wa Ushuru na Forodha (FIATA) Bw. Turgut Erkeskin amesifu juhudi zinazofanywa na Tanzania Bara na Zanzibar katika kuboresha sekta ya forodha.

EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"