Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) IJP Mstaafu Balozi Ernest Mangu( Picha ya kwanza ameketi katikati suti ya dark blue) na Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw. Plasduce Mkeli Mbossa( Picha ya pili) wakiwa katika kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma ( CEOs Forum 2025), kinachofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha ( AICC).

Kauli mbiu katika Kikao kazi hicho ni “ Ushirikiano endelevu wa Biashara katika Mazingira ya ushindani wa kimataifa, nafasi ya Mashirika ya Umma”. 

Mgeni rasmi ni Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango, akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Uchaguzi 2025 Logo