Mwandishi Wetu

Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imeipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa kuendelea kuboresha huduma zake katika Bandari zake na kufanya Wafanyabiashara kuendelea kufurahia huduma na kuendelea kutumia bandari za TPA.

Pongezi hizo zimetolewa tarehe 25 Novemba,2024 kupitia Risala yao iliyosomwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kanda ya Ziwa Victoria Bw. Nicholaus Basimaki, katika Mkutano wa 10 wa mwaka 2024, uliofanyika Ukumbi wa Ubungo Plaza Jijini Dar es Salaam.

TPA ilikuwa ni miongoni mwa Wadhamini wa Mkutano huo wa siku moja umeshirikisha Wajumbe 400 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.