Mamia ya Wananchi na Wadau wa Bandari wamejitokeza kwa wingi katika Banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ( Sabasaba) ili kupata elimu kuhusu shughuli mbalimbali za utekelezaji bandarini na kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na Mamlaka.