Matukio mbalimbali katika picha wakati Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Bw. Ludovick Nduhiye, alipotembelea bandari za Mwanza Kaskazini, Kemondo na Bukoba, tarehe 05 na 06 Machi, 2025 kukagua na kujionea utekelezaji wa miradi ya maboresho na upanuzi wa bandari hizo.

Bw. Nduhiye ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) kwa usimamizi makini na ufanisi wa miradi ya upanuzi na uboreshaji wa bandari hizo ambayo ni jitihada za Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) katika kuboresha hali ya usafiri na usafirishaji ndani ya Ziwa Viktoria.