TPA YASHIRIKI MAONESHO YA WAKULIMA (NANENANE) JIJINI DODOMA

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Dkt.Ladislaus Chang’a ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa ufanisi na uweledi katika kuhudumia Shehena.
Dkt.Chang’a ametoa kauli hiyo Agosti 04,2025 alipotembelea banda la TPA lililopo katika Viwanja vya Nzuguni Dodoma yanakofanyika Maonesho ya Wakulima (Nanenane)
Banda la TPA limekuwa kivutio katika Maonesho hayo yanayotarajiwa kufikia kilele Agosti 08, 2025 kwa watu wa rika tofauti kutembelea kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yahusuyo sekta ya Uchukuzi.