WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA KATIKA BANDARI YA LINDI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akiwa katika ziara yake inayoendelea Mkoani Lindi, tarehe 21 Disemba 2025 ametembelea Bandari ya Lindi na kujionea shughuli mbalimbali za utekelezaji katika Bandari hiyo.
Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri Mkuu alipokea taarifa fupi ya utendaji kazi wa Bandari ya Lindi kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Mtwara Bw. Ferdinand Nyathi ambaye alieleza kuhusu hali ya uendeshaji wa Bandari ya Lindi, mafanikio yaliyopo pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili Bandari hiyo kwa sasa.
Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack ameeleza kuwa, Bandari ya Lindi inakabiliwa na changamoto ya kujaa mchanga katika eneo la gati hali inayosababisha kupungua kwa kina cha Bandari na hivyo kuathiri uwezo wa kuhudumia meli hususan meli za mizigo mchanganyiko ambazo zinahitaji uwepo wa kina kirefu.
Baada ya kupata maelezo yote hayo, Mhe. Waziri Mkuu alitoa maagizo kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuharakisha mchakato wa kufanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Bandari mbadala.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"