Maofisa wa kijeshi kutoka nchini Nigeria wakiongozwa na Air Vice Marshal Titus Z. Dauda wamefanya ziara katika Bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza masuala ya kiuchumi, siasa na kiutamaduni pamoja na mchango wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania TPA katika maendeleo ya Kiuchumi nchini Tanzania.

Pamoja na Mambo mengine ujumbe uhuo ulipata fursa ya kutembelea kujionea shughuli za bandari ikiwemo gati ya kuhudumia magari 'Roro Terminal " Pamoja na gati 1-7

Ujumbe huo ulipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed G. Abed kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu TPA Bw. Plasduce M. Mbossa.