Katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani, Wanawake watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania( TPA) ,tarehe 12 Machi 2025, wameshiriki matendo ya huruma kwa kutoa misaada ya vifaa tiba katika hospitali za Wilaya ya Kigamboni na Temeke vyenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 49.
Akipokea vifaa tiba hivyo vya aina 15 tofauti, Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Halima Bulembo amesema hii si mara ya kwanza kwa TPA kutoa misaada katika Wilaya hiyo,na kwa kitendo hicho anaishukuru sana Menejimenti ya TPA.
Akizungumza wakati anakabidhi vifaa tiba hivyo.Meneja Rasilimali Watu wa Bandari ya Dar es Salaam Bi.Mwajuma Mkonga, amesema TPA imetoa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 24 katika hospitali ya Kigamboni na katika hospitali ya Rufaa ya Temeke wametoa vyenye thamani ya shilingi milioni 25.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Temeke, Daktari Bingwa wa macho Annamary Rugakiza Stanslaus, ameishukuru TPA hususani Wafanyakazi wanawake kwa msaada wao ambao utaenda kuwasaidia kwa kuokoa maisha ya wakinamama na watoto wachanga.

Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Machi 11,2025 imekutana na Wafanyabiashara kutoka nchini Uholanzi katika jengo la Makao Makuu ya TPA Jijini Dar es Salaam, ili kujadiliana juu ya fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kibiashara katika Bandari.
Ujumbe wa Wafanyabiashara hao kutoka kampuni za Invest International, Korpershoek na Ramco International ulipokelewa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dkt. Baraka Mdima kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu Bw. Plasduce Mbossa.
Meli ya MV AFRICAN DIPPER yenye urefu wa mita 179.9, tarehe 10 Machi,2025, imewasili katika Bandari ya Mtwara ikitokea nchini Uturuki ikiwa na shehena ya Sulphur, tani 9,202.54 ( Elfu tisa mia mbili na mbili nukta tano nne)
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Kanali Michael Mtenjele ameongoza mapokezi ya meli hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Kenan Sawala ambapo ametoa wito kwa Bodi ya Korosho kuhakikisha kuwa Sulphur hiyo inasambazwa kwa wakati kwa wakulima ili kuleta tija katika uzalishaji wa zao la Korosho.
Naye Meneja wa Bandari ya Mtwara Bw. Ferdinand Nyathi amesema Bandari ya Mtwara imejipanga vema kwa rasilimaliwatu ya kutosha, vitendea kazi na mitambo ili kuhudumia shehena mbalimbali ikiwemo Sulphur.
Watumishi Wanawake wa Bandari ya Mtwara wameungana na wanawake wote Duniani katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo Mjini Mtwara.
Maadhimisho hayo yameongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bw. Abdallah Mwaipaya ambaye ametoa wito kwa Wanawake wote kuungana katika kushiriki shughuli za maendeleo.
Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani, wafanyakazi wanawake wa Bandari ya Tanga wametoa msaada wa vifaa mbalimbali wenye thamani ya Tsh 5,419,000 katika kituo cha “Goodwill Children’s Home “kilichopo kata ya Mwahako Wilaya ya Tanga mjini.
Sambamba na kukabidhi msaada huo wanawake hao walijumuika na watoto hao katika futari maalumu iliyoandaliwa na wafanyakazi hao katika viwanja vya Club ya Bandari.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga Bw. Peter Millanzi, aliwapongeza wanawake hao kwa kufanya matendo ya huruma kwa watoto hao katika mwezi mtukufu wa Ramadhani jambo ambalo ni baraka na faraja kwa wenye uhitaji.
Awali wanawake hao walishiriki kwenye maandamano ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambapo Wilaya ya Tanga mjini maadhimisho hayo yamefanyika tarehe 5 Machi ,2025 na kauli mbiu ya mwaka 2025 ni “ Wanawake, Wasichana 2025 Tuimarishe Haki , Usawa na Uwezeshaji”
- WAFANYAKAZI WA TPA WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KIMKOA VIWANJA VYA LEADERS CLUB KINONDONI DAR ES SALAAM
- NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA UCHUKUZI ATEMBELEA BANDARI ZA MWANZA KASKAZINI
- ZIARA YA MAOFISA WAKIJESHI KUTOKA NCHINI NIGERIA KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM
- TAARIFA KWA UMMA (UFAFANUZI JUU YA TAARIFA ZISIZO SAHIHI ZA MZIGO INAYOPITA BANDARI YA KIGOMA)
EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"