Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, tarehe 13 Agosti 2025 amekagua mabasi 99 ya Kampuni ya Mofat katika Bandari ya Dar es Salaam na kuwaagiza kuanza kutoa huduma ya usafiri ndani ya siku 7.
Mabasi hayo yatatoa huduma katika njia ya kuanzia katikati ya Jiji la Dar es Salaam kwenda Mbagala.
Mhe. Majaliwa ameishukuru Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa kuwezesha magari hayo kushushwa Bandarini kwa haraka na kuhifadhiwa kwa muda katika yadi ya magari (RoRo).
Kwa kuwa taratibu zote za kibandari zimekamilika, Mhe. Waziri Mkuu amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mofat Bw. Abdallah Kassim kuyaondoa mabasi hayo kwa wakati ili kutoa nafasi ya kuhudumia mizigo ya Wateja wengine.
Mhe. Waziri Mkuu aliambatana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, na Uratibu) Mhe. William Lukuvi , Naibu Waziri wa Tamisemi Mhe. Zainab Katimba, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi, Mkurugenzi Mkuu wa (DART) Dkt. Athuman Kihamia, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolona na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.
Mara baada ya kufika Bandarini, Mhe. Waziri Mkuu amepokelewa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mha. Dkt. Baraka Mdima kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu TPA Bw. Plasduce Mbossa, pamoja na Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed Gallus na watendaji wengine wa Mamlaka.




Katibu Mkuu wa Chama cha Usimamizi wa Bandari Mashariki na Kusini mwa Afrika (Port Management Association of Eastern and Southern Africa-PMAESA) Kanali Andre Didace Ciseau amekutana na Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) katika kikao kilicholenga kuimarisha uhusiano baina ya pande hizo mbili.
Kanali Ciseau amesema PMAESA inatambua na kuthamini mchango wa TPA kama miongoni mwa taasisi zenye uwezo mkubwa kiutendaji katika Ukanda wa Kusini na Mashariki mwa Afrika.
Akizungumza katika Kikao hicho Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dkt. Baraka Mdima ameeleza mipango ya muda mfupi na mrefu ya TPA na utayari wa Mamlaka kuendelea kuimarisha ushirikiano wake na PMAESA.




Wakuu wa Taasisi mbalimbali za Umma kwa nyakati tofauti wametembelea Banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) katika Maonesho ya 32 ya Wakulima (Nanenane) yanayofikia tamati leo katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma na kuipongeza Mamlaka kwa ufanisi na mchango wake kwa Taifa kiuchumi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) CPA Habibu J. Suluo ametoa pongezi zake kwa kusema wanatambua na kuthamini mchango wa TPA katika uchumi na kijamii.
Naye Kamishna wa Bima kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Dkt. Baghayo Saqware,amesema anatambua mchango wa TPA kwa uchumi wa nchi na umuhimu wa bidhaaa zinazoingia nchini kukatiwa Bima.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bwa.Salim Msangi ameipongeza TPA kwa ufanisi wa kuhudumia shehena.









Chuo cha Bandari kinaendelea kutumia fursa ya ushiriki katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) kukutana na kutoa maelezo ya mafunzo yatolewayo na umuhimu wake,kwa wazazi na wanafunzi wa shule mbalimbali zilipo mjini Dodoma na mikoa ya jirani waliotembelea banda la TPA lililopo viwanja vya Nzuguni




Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Said Jafo ametembelea Banda la Bandari ya Mtwara katika kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi (Nanenane) ambayo yamehitimishwa rasmi tarehe 08 Agosti, 2025 katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mhe.Dkt. Jafo ameelezea kuvutiwa na utayari wa Bandari ya Mtwara katika kuhudumia shehena mbalimbali ikiwemo mazao ya kilimo kama korosho.
Aidha, ameipongeza Mikoa ya Lindi na Mtwara kwa kufanya maandalizi mazuri ya maonesho hayo ambapo yamekuwa ya mvuto mkubwa kwa Wananchi.


- TPA YASHIRIKI KATIKA MKUTANO WA TATU WA UMOJA WA MATAIFA WA NCHI ZISIZO NA BAHARI (LLDC3)
- MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM ATEMBELEA BANDA LA BANDARI YA TANGA MAONESHO YA NANE NANE MOROGORO
- MKUU WA MKOA MTWARA ATEMBELEA BANDA LA MTWARA KATIKA MAONESHO YA WAKULIMA MKOANI LINDI
- NAMPORT WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM
EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"